Jumatatu, 1 Februari 2016

WIFE KAKUTANA NA EX WAKE KAFURAHI HAKUNA MFANO!

Wadau mambo vipi?
Kuna jambo limeikoroga akili yangu sana juzi naomba niwashirikishe kidogo. Jumamosi iliyopita mimi na wife tulienda kula bata maeneo ya Villa Park hapa  Mwanza nyakati za jioni baada ya kutoka kufanya shopping hapo Rock City Mall maeneo ya Ghana. Wakati tumefika maEneo ya Nyegezi tukielekea mjini wife alinambia nisimame kidogo kuna rafiki yake yupo saloon ambaye nilikua namfahamu tangu wakiwa chuo Saut  Nyegezi , nae alikua anaelekea hukohuko Rock cCity Mall tumchukue, akampigia girlfriend simu aje barabarani . Hivyo tukawa watatu kwenyegari mpaka  mizunguko ya huko mall; mimi, wife na girlfriend ambae alikua family friend kwetu ingawa mimi sina mazoea nae kiiivile.
Kwa kuwa ilikua mida ya saa kumi na moja jua lilipoanza kuzama tukaamua kukaa Villa Park kwa ajili ya kusubiri kusakata rhumba na kwa kuwa wwife huyu alikua ni shaga yake hasa sikua na option zaidi ya kuwaacha wahe huru uku mimi nikiendelea kugonga Konyagi yangu kubwa na better lemon  na wao walikua wanakunywa Saint Anna moja wawili, tukakaa karibia na kaunta ya chini  nje. Kwenye saa mbili kasoro usiku akajitokeza jamaa mmoja kwa sura simjuhi kabisa ,baada ya kutuona akaja kutusalimia, ambapo wife aliinuka kwa shangwe kubwa na kumlaki kwa hugs na zile kiss za mashavuni wanazopiganaga wale wanaojifanya wazungu,jamaa likamkumbatia wife kwa nguvu.Nilipata kawivu kidogo lakini nikajikaza kiume!
Wife akanitambulisha kuwa "he is a longtime friend,huku nikiendelea kumtazama kwa mashaka kwani nilihisi zile mbwe mbwe zote za kukumbatiana pale kuwa sio ‘genuine’ lazima kuna kitu au kulikua na kitu fulani zamani,haiwezekani,hamna hapana!kuna kitu tu!". Jamaa akaita weita na akazungusha mbili za vinywaji, alafu akaniomba aende akamtambulishe wife kwenye meza yao kwa rafiki zake ,sikupendelea hiyo hali lakini kwa kuwa nilimuona wife ana muhemko fulani wa bashasha ya kukutana naa “friend wa zamani” nikakubalitu kwa shingo upande  ingawa moyoni nilikua nimefura kwa hasira, sema sikutaka kuonesha, bahati mbaya zaidi meza ya hiyo aliyokua ametokea huyo jamaa  ilijaa wanaume pekee.
Tukabaki wawili wakati wife anaongea na meza ile, yule girlfriend akasema "shemeji naomba namba yako hapa mjini huwezi kujua ya kesho na keshokutwa", nami nikajibu ni kweli kabisa, tukabadilishana namba.Monday yule binti akanipigia simu nikiwa kazini akaniambia shemeji kuna jambo nataka kukuambia ila usinitaje, nikajibu poa, akasema, "Yule jamaa wa jana ni ex wa mkeo. Walikua wapenzi kwa miaka yote mitatu chuoni wakiishi chumba kimoja nje ya chuo kama mke na Mume".
Na kwamba kwa kipindi chote cha hiyo 3 yrs alitoa kama mimba 2 hivi za huyo mshikaji, pia uhusiano wao ulienda hadi mtaani after university life. Walikuja kuachana kila mtu alipopata kazi yule ndugu akapelekwa Songea. Since then hawajawahi kuonana hadi hiyo jumapili pale Lock City Mall,Mwanza na kwamba ile njemba limerudishwa hapa Mwanza na halijaoa bado ila lina mapene sana.
Binti huyu alinibembeleza sana kuwa nisimtaje kabisa kama yeye ndie source ya hiyo habari. Huyu binti ni rafiki wa wife tangu chuo ila bahati mbaya ndoa yake ilipata shida kidogo na kushindikana kutokana na uzinzi wa mwanaume.Niliporudi home jioni ya monday nikaamua kulianzisha, ambapo wife alidai hakuona busara kunitambulisha kwamba yule bwana alikua ex wake.
Nikamuuliza ilikuaje ukafurahi na kushangilia kiasi kile na kushindwa kuficha kabisa hisia zako? Akabaki anajiuma uma tu na kushindwa kujibu.
Kiukweli sijaridhika na majibu yale na bado nafanya uchunguzi.



Maoni 2 :

  1. Ushuhuda Wangu wa Kutoka Moyoni 💖

    Baada ya baba yangu mdogo kuniacha kwa miezi saba mirefu, nilikuwa nimevunjika moyo kabisa. Alinizuia kwenye mitandao yote ya kijamii, akaondoka, na hakukuwa na njia ya kumfikia. Karibu nikate tamaa, lakini ndani kabisa nilijua singeweza kupata mtu yeyote ambaye angenipenda na kunitendea jinsi alivyonitendea.

    Siku moja, bosi wangu kazini aligundua jinsi nilivyokuwa na huzuni na akanitambulisha kwa Dkt. Dawn. Dkt. Dawn alisikiliza hadithi yangu na akaahidi kwamba mpenzi wangu angerudi kwangu ndani ya siku tatu. Kwa kweli, sikuamini mwanzoni—lakini kwa mshangao wangu mkubwa, siku ya tatu simu yangu iliita. Ilikuwa yeye! Alikuwa akilia na kuomba msamaha, akisema hataniacha tena.

    Tangu siku hiyo, uhusiano wetu umekuwa na nguvu na uzuri zaidi kuliko hapo awali. Amekuwa akipenda na kunijali mimi na mtoto wetu, na sasa tunafunga ndoa katika miezi miwili tu! ❤️

    Shukrani zote kwa Dkt. Dawn, ambaye kwa kweli alifanya jambo lisilowezekana liwezekane. Ninampendekeza kwa moyo wote kwa yeyote anayekabiliwa na changamoto katika:

    Masuala ya uhusiano au ndoa

    Ugonjwa au magonjwa

    Matatizo ya utasa au bahati nasibu

    Kesi za mahakamani au urejeshaji wa mali

    Dkt. Dawn kweli hutatua matatizo kwa ufanisi na hurudisha furaha katika maisha ya watu.

    Wasiliana na Dr. Dawn kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    JibuFuta
  2. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
    dawnacuna314@gmail.com

    JibuFuta