Weekend iliyopita nilitoka na jamaa yangu aliyenitembelea,
tukaenda sehemu moja iko busy sana jina nalihifadhi. Kuna live band, club,
vyakula na vinywaji almost kila variety.
Kina dada hujichanganya sana kwenye eneo hilo. Jamaa yangu
huyo ni mpenzi wa mambo yetu yale, hivyo kadri alivyokuwa akipata moja baridi
ndivyo ari ya kupata kimwana mmojawapo ilivyokuwa inaongezeka.
Baadaye aliamua kumwita mhudumu amwitie kimwana aliyekuwa
amevutiwa naye.
Walikwenda pembeni kidogo kujadili, baadaye jamaa yangu huyo
akarudi akaniambia amekubaliana kwenda kumgegeda huyo kimwana lakini akaomba
kwa vile sio mwenyeji nimpeleke lodge.
Nikampa ufunguo ili watangulie kwenye gari, baadaye nilikwenda
na kuwakuta wamo ndani ya gari tayari, nilimsalimia huyo kimwana, sauti yake
ikawa sio ngeni masikioni mwangu. Nilipogeuka sikuamini macho yangu kuwa ni mke
wa jirani yetu mtaani. Sikuwa na la kufanya zaidi ya kumwambia jamaa yangu aje
aendeshe gari mwenyewe, Nikatoa udhuru. Jamaa yangu alinipa mrejesho kapewa
mambo si kawaida.
Sasa ninachojiuliza ni kuwa kumbe hata wake za watu
wanajiuza?
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni