Jumanne, 2 Agosti 2016

KUMBE WAKE ZA WATU NAO WANAJIUZA?

Weekend iliyopita nilitoka na jamaa yangu aliyenitembelea, tukaenda sehemu moja iko busy sana jina nalihifadhi. Kuna live band, club, vyakula na vinywaji almost kila variety.

Kina dada hujichanganya sana kwenye eneo hilo. Jamaa yangu huyo ni mpenzi wa mambo yetu yale, hivyo kadri alivyokuwa akipata moja baridi ndivyo ari ya kupata kimwana mmojawapo ilivyokuwa inaongezeka.

Baadaye aliamua kumwita mhudumu amwitie kimwana aliyekuwa amevutiwa naye.

Walikwenda pembeni kidogo kujadili, baadaye jamaa yangu huyo akarudi akaniambia amekubaliana kwenda kumgegeda huyo kimwana lakini akaomba kwa vile sio mwenyeji nimpeleke lodge.

Nikampa ufunguo ili watangulie kwenye gari, baadaye nilikwenda na kuwakuta wamo ndani ya gari tayari, nilimsalimia huyo kimwana, sauti yake ikawa sio ngeni masikioni mwangu. Nilipogeuka sikuamini macho yangu kuwa ni mke wa jirani yetu mtaani. Sikuwa na la kufanya zaidi ya kumwambia jamaa yangu aje aendeshe gari mwenyewe, Nikatoa udhuru. Jamaa yangu alinipa mrejesho kapewa mambo si kawaida.


Sasa ninachojiuliza ni kuwa kumbe hata wake za watu wanajiuza?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni