Kuna shemeji yangu ambaye nimezaa na mdogo wake wa kike
ameolewa ni mzuri na amejazia sana tumekuwa na mahusiano ya siri ya kupeana
mgegedo tangu 2014 pindi baada ya mdogo
wake kuamua kuhama Dar na kurejea Tunduma kwao ambapo aliolewa na bwana mwingine.
Mume wake huwa namuita kaka maana amenizidi umri na pia kwa kuwa
ameoa dada wa demu wangu.
Huyu mumewe ni mtu mpole na mkarimu sana ni fundi magari hivyo huwa tunamwita kutengeneza
kidaladala chetu kinapoharibika na huwa natumia mwanya huo kwenda “ kummega” mkewe.
Jumapili iliyopita nilimpigia simu aje kutengeneza gari(mimi
naishi Kinyerezi nayeye anaishi Jet. Akaja nikamwambia akague gari ili
nimwachie hela kwa ajili ya kununua vifaa.Alifanya hvyo akanipa hesabu ya
spares nikamwachia hela na nikamsisitiza kwamba akimaliza kutengeneza afanye
test ya gari ikibidi hadi Mbezi.
Lengo langu likiwa akianza kutengeneza gari na ule muda wa
kutest niwahi fasta nyumbani kwake kula uroda shemeji yangu.Wakati anafuata
spare Ilala mi nikamuaga kwamba naenda Tegeta hivyo tutawasiliana akimaliza
matengenezo.
Mwanaume nikaenda zangu Jet ambapo nilimkuta shemeji ameshajifukizia
udi kwa ajilia ya masham sham ya sita kwa sita mle ndani kwake.Tukafanya yetu huku tukiamini
jamaa yupo bize na gari hivyo akimaliza lazma atanipigia kunijulisha.Nami kila
mara nikawa nampigia kumuulizia alipofikia,bahati mbaya mara ya mwisho kumpigia
hakupokea simu nikaamini atakuwa anatest gari maeneo ya Kinyerezi alipokuwa
akiitengeneza.
Lahaula kumbe jamaa aliamua kutest gari kuja nyumbani kwake
Jet bahati mbaya au nzuri nilishapiga bao zangu mbili tukakaa na shemeji
sebuleni huku nimevaa singlend.
Ghafla jamaa kaingia ndani katukuta tumekaa sebuleni na wife
wake akasalimia akanipa feedback na kunieleza kaja na gari ipo nje.
Kwakweli nilifedheheka sana kwakuwa nilimuaga jamaa naenda
Tegeta nasasa kanikuta kwake.Nilimpa hela yake ya ufundi tena kwa kumzidishia
amount ili kuficha aibu na jamaa alipokea lakini hakuwa sawa kama nilivyomzoea.
Sasa ndugu zangu nafsi inanisuta kwa kumuibia jamaa mke wake
ukizingatia ndio fundi wetu na huwa anatusaidia kwa mengi kiufundi.
Nikiwasiliana na shemeji yangu anadai jamaa hajamuuliza
chochote ila kwa upande wangu sijaridhika kabisa nahisi jamaa alihisi mchezo
mbaya hivyo kukaa kimya tu.
Wadau nifanyeje nikimpigia simu kuhusu gari anapokea na kunipa
maelekezo kama kawaida kama vile hakija tokea kitu chochote.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni