Jumatatu nilikwenda kazini kwa mke wangu kuchukua ufunguo wa
nyumbani kuna kitu nilisahau nyumbani hivyo niliitaji kukirudia, yeye ndo huwa
anawahi kurudi nyumbani so huwa anakaa na ufunguo, wangu nilipoteza kwenye
pombe.Sikua nimempigia simu nilijua atakuwepo tu kazini.
Nilipofika pale nilielekezwa na watu wa mapokezi chumba cha
ofisi anamofanyia kazi. Unexpectedly, nilipofungua tu mlango wa chumba hicho
nikakuta jamaa mmoja staff mwenzie na wife akimpiga vibao wife kwenye wowowo
nalopumzikia mimi huku wife akifurahia kitendo kile na staff wote mule
wakifurahia. Yule bwana aliendelea na zoezi hilo huku wife amekinga wowowo na
staff wakiendelea kufurahia tukio hilo.
Wakati huo mimi nimeganda mlangoni kwa mshangao mkubwa
nikijiuliza hili lijamaa litakua halijapata kweli? Hadi kufikia hatua hiyo?
Wife alipogeuka mlangoni akakutana uso kwa uso na mimi almanusura azirai,
alitweta, jasho jingi lilimtoka, wale staff mle ndani hawanifahamu hivyo
hawakujua kinachoendelea, nikafunga mlango taratibu na kuondoka kwenda kwenye
lift, wife akawa ananikimbilia kwa nyuma kimya nadhani kwa kuogopa staff
wengine wasijue chochote.
Nilipoingia kwenye Gari akaanza kuomba anielezee sikumpa
nafasi hiyo nikawasha Gari na kuondoka nikarudi usiku wa manane home,
nikamwambia park vitu vyako asubuhi pakikucha uondoke sikutaki tena alilia sana
alikesha ananibembeleza nisimwache kwamba ulikua ni utani tu wa ofisini hawana
uhusiano wowote na yule jamaa, kwamba tumpigie hata simu na wengine pia pale
ofisini.
Nikamjibu kwamba sihitaji kuelezewa nimeona kwa macho yangu,
na kwamba kuwepo na mahusiano au kusiwepo kwangu sio tija sana,
linalonisikitisha ni mke wa mtu kukosa adabu kiasi kile na kujirahisisha kwa
wanaume, kushindwa kujiheshimu na kuruhusu mwanaume mwingine akupige kofi
kwenye makalio ndio dhambi kubwa katika sakata hili.
Kwa tabia hii wanaume wote office nzima watakutongoza
wakiamini ww ni maharage ya mbeya, hivyo sikutaki tens
Nikamjibu hivyo. Amengangania kwangu tangu siku hiyo hataki
kuondoka akiomboleza na kuomba msamaha, ingawa sisemi nae chochote tangu siku
hiyo bado namvutia kasi.
Huyu mwanamke hatujafunga ndoa, ila tunaishi tu, nilimleta
hili kum replace mke wangu wa kwanza tulieachana kwa talaka mahakamani kutokana
na mimi kushindikana kwa uzinzi nina watoto na mtalaka wangu ambao tunasomesha
pamoja
ni muda tangu tulipoachana ila haachi kusisitiza turudiane
tulee watoto pamoja, anadai ndugu yake wakili ndie aliemchochea kuomba talaka
miimi nilishindwa kurudiana nae kutokana na guilty conscience kwa matendo
niliyomtendea
Sasa waheshimiwa huyu nilie nae sasa nilimwambia nakupa
probation niweze kuiona tabia yako, maana katika mazingira yasiyoeleweka akawa
akija kwangu anaacha nguo hadi kufikia begi mbili ndivyo tulivyoanza kuishi
hivyo.
Kwa hili nililoliona si ameshindwa probation huyu? Maana
nimeamua kuwa mtu mzuri na kuacha mabaya yote yaliyosababisha nishindwane na
familia yangu.Hebu nisaidieni suluhisho
Way forward please!?
Fredy:
1. Kushikwa makalio
ndo alama ya wao kuwa na mahusiano?
2. Kushikwa makalio ndo alama ya kwamba atatongozwa na kila
mu ofisini kwake? Kwani asiposhikwa hawezi tongozwa?
3. Kwanini hujampa nafasi ya kumsikiliza ili uwe fair kwenye
maamuzi?
4. Unadhani kumtimua ndo suluhisho la hali unayopitia?
5. Haya, let us say umemtimua, una uhakika gani utakayemleta
hatayafanya hayo au zaidi ya hayo?
6. Haya, let say umebadili wanawake mara kadhaa, na wee
hujabadilishwa, do you think wenye matatizo ni hao wanawake au ni wewe? You
know sometimes binadamu huwa tunakimbia vivuli vyetu... tunasahau kuwa jua
likiwaka tu, kivuli hichooooooo....
Waza kwa kina hayo maswali... Utapata majibu!
SALUM:
Inategemea ulikutana nae wapi Mkuu; kwa
utamaduni wa kiafrika ni aibu na fedheha kubwa kwa mwanamke potelea mbali mke
wa MTU kushikwa makalio tena mbele ya hadhara ya watu! huo ni upungufu mkubwa
wa Maadil! Acha uzinzi rudia mke wa zaman Mkuu