Ijumaa, 24 Juni 2016

WANAWAKE:VAENI NGUO ZA KUSITIRI MIILI YENU

Sijui ni masifa au nini ila kwa kweli sio vyema kabisa unamkuta mdada kavaa nguo ndefu tu ila tatizo ni transparent zinaonyesha hadi chupi na sehemu nyingine za maungo yao kweli sio vizuri wanaume tunapata wakati mgumu sana kwani nguo zenu zinatuhamasisha kufanya ngono na vitendo vingine vya kichochezi.
Ni hali ngumu sana unapokatiza mjini/mtaani/shule/vyuoni/daladala unakutana na haya maafa kwa kweli wanawake mnatumaliza sisi wanaume.Nidhamu ya mavazi ichukue mkondo mavazi yenye kuonyesha sehemu za ndani yaachwe pia nguo zinazobana zinaonyesha hadi mistari ya chupi ziachwe nasema tena maana hamna namna hata hizi fupi zinazoonyesha mapaja na viuno mziache mwanamke vaa vazi kubwa la kufunika na kusitiri mwili wako wote.
Mi langu rohoni leo nalitua,ukweli nakereka na kujiskia aibu kwa hili.Yani unakuta mdada au hata mwanamke mtu mzima anafanya makusudi kuingia kwenye shughuli za watu za heshima zinazohitaji mavazi ya kujisitir angalau basi nguo iishie magotini na kuficha sehemu nyeti na kama matiti na mapaja...
Ye utakuta kaingia na kigauni utadhani cha mtoto wa shule ya msingi miziwa yote ipo nje nje..Mipaja yake nusu na robo ipo nje,sasa hapo hata akiangusha kitu sidhan kama ataweza okota!Alafu kihelehele uyoooo anaomba asevu high tabo!
Sasa hebu fikiria watu wanafanya shughuli ya kumuaga binti yao (send off) au harusi ukumbini..kule mbele kuna wazaz na wazee wetu wengine wa heshima,upande mwingne wamekaa wakwe..
Muda wa kucheza mziki unaingia pale mbele kwa mbwembwe zote shost unajimwaga ukiwa nusu uchi na kutuaibisha wanawake wenzio hadi tunaona aibu,mi nlishuhudia zaidi ya sherehe moja..
Tena mdada anawapa mgongo wazazi wa yule shogake anayeagwa uchezaji wenyewe wa kujibinua ka' mbuzi anetolewa kafara,huku nyuma mipaja yote nje bado sentimeta moja matako yaonekane,mama mzaz akainamisha kichwa pale kwa aibu ya anachoona.
Mi nnachoomba angalia dressing code yako kwa eneo husika,sio unavaa mradi kiende.Utavaaje kigauni cha klabu kwenye wedding reception zetu za kitanzania? halafu ukiangalia nyomi lote walovivaa unakuta ni ww au kuna mwingne pemben ndo mlovaa kiaibu tu..

Hata kama ni kwenda na fashion zingatien mahali mnakoenda hata kama hakuna wazaz au wazee wenu bado waliopo watawachukulia kivingine tu!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni