Naomba niongee nanyi waume zetu jamani, hebu tulieni na wake
zenu maana cha zaidi mnachokitafuta ni aibu na magonjwa.
Nikiwa saloon (kama mnavyojua mambo ya saloon full umbeya
hakuna siri) wadada wakawa wakiongea, mmoja anatembea na mume wa mtu akasema
"yaani yule boya kweli mi nataka hela zake tu,kitandani hana kitu
kabisa,yaani kimoja tu tena cha dakika moja tu yuko hoi,ananichafuaga lol na
ule mtumbo wake anajiburuza tu kama nyoka. Namuonea huruma mkewe maana alivyo
mzuri, bora mimi nina jamaa yangu wa kunikuna,sasa mkewe sijui anafanyaje masikini"!
Wakacheka wote kwa mkupuo na kuendelea kuwaongelea wanaume
in general na wakitoa shuhuda zao za vituko wanavyokutana navyo.Sio siri
nilijikuta naumia nafsi kama ndio mimi vile,nikawaza hiyo aibu.
Hivi mnajijua uwezo hamna,ni nini sasa mnachokitafuta?
Au ni kwamba hamyajui hayo madhaifu yenu,au mnataka nanyi
muonekane vidume? au...... au...... najikuta tu nabaki na au au.
Na wanawake wenzangu tujitahidi kwenye masuala ya misosi na
kuwashauri mazoezi,tusiruhusu hivyo vitambi vyao, mume wangu nimemtengenezea
kabisa ratiba ya kula na bahati nzuri hapendi kitambi so na mazoezi anafanya
japo mvivu sometimes, so huwa namsisitiza sana kuhusu mazoezi na ikiwezekana
tunafanya wote.
Nanyi wanaume hebu mfunge zipu,majaribu yapo ila mshindeni
shetani myashinde.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni