Ijumaa, 24 Juni 2016

WANAUME ZETU MNATUTIA AIBU,MTULIE

Naomba niongee nanyi waume zetu jamani, hebu tulieni na wake zenu maana cha zaidi mnachokitafuta ni aibu na magonjwa.
Nikiwa saloon (kama mnavyojua mambo ya saloon full umbeya hakuna siri) wadada wakawa wakiongea, mmoja anatembea na mume wa mtu akasema "yaani yule boya kweli mi nataka hela zake tu,kitandani hana kitu kabisa,yaani kimoja tu tena cha dakika moja tu yuko hoi,ananichafuaga lol na ule mtumbo wake anajiburuza tu kama nyoka. Namuonea huruma mkewe maana alivyo mzuri, bora mimi nina jamaa yangu wa kunikuna,sasa mkewe sijui anafanyaje masikini"!
Wakacheka wote kwa mkupuo na kuendelea kuwaongelea wanaume in general na wakitoa shuhuda zao za vituko wanavyokutana navyo.Sio siri nilijikuta naumia nafsi kama ndio mimi vile,nikawaza hiyo aibu.
Hivi mnajijua uwezo hamna,ni nini sasa mnachokitafuta?
Au ni kwamba hamyajui hayo madhaifu yenu,au mnataka nanyi muonekane vidume? au...... au...... najikuta tu nabaki na au au.
Na wanawake wenzangu tujitahidi kwenye masuala ya misosi na kuwashauri mazoezi,tusiruhusu hivyo vitambi vyao, mume wangu nimemtengenezea kabisa ratiba ya kula na bahati nzuri hapendi kitambi so na mazoezi anafanya japo mvivu sometimes, so huwa namsisitiza sana kuhusu mazoezi na ikiwezekana tunafanya wote.

Nanyi wanaume hebu mfunge zipu,majaribu yapo ila mshindeni shetani myashinde.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni