Leo hii tutaona aina kumi za ndoa kama ifuatavyo:
1. NDOA YA MKEKA
Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu.Ndoa hii huwa Haina
mahari. Hii huvunjika mwaka mmoja tu,baada ya wanandoa kugundua hawakuwa
wakipendana!Ni maarufu sana kwenye miji ya Pwani san asana uswahilini.
2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)
Hufungwa na vijana wa kiume wenye umri wa miaka kati mume 22 mpaka 25 na mke miaka
19 mpaka 23.Mara nyingi vikao vya harusi uanza pindi kijana anapokuwa amepata
kazi baada ya kumaliza elimu ya chuo na uvunjika baada ya miaka 2 au 3 ya ndoa,kwani
wanandoa wanakua sio wakomavu(mambo mengi ya mihemko kama vile kuchepuka nje ya
ndooa wanakuwa hawana uzowefu nayo).
4. NDOA YA MAONYESHO
Wenye ndoa hii hupenda kujionyesha barabarani na mara nyngi
wanandoa hasahasa wanawake ufose kingi aolewe kwa ajili ya mashindano tu na
shoga yake kwasababu nao wameolewa basi nayeyey lazima aolewe tu ili kuondoa
mkosi tu,na mara nyingi ndoa inakuwa ni ya ukumbini tu lakini rohoni hamna kitu.Ila
ndani hazina utii.Hupigana kila wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha
kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa zinazoongoza kwa kuchepuka!
5. NDOA YA UHAMISHO.
Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa kijijini
ahamie mjini.Mahari utoa anaetaka kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume
lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi
wote mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini kwenda kijijini.
6. NDOA YA MIMBA.
Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki kuonekana makwao
kuwa wamezaa nje. Au muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa dhati.Mara nyingi muolewaji
hutumia mimba kama mtego wa kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na
kufikisha mwaka 1 au 2.Mara nyingi utengenezwa na mabinti wa mjini hasahasa
wasomi au wenye kipato na kazi nzuri.Hapa mara nyingi
muolewaji anakua ameshapata kila kitu katika maisha kasoro mume tu!
7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)
Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa hii pia huitwa
ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni
mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa hizi hulea watoto wasio wao.
8. NDOA YA KWASABABU.
Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji aonekane tu kwa jamii
kuwa naye kaoa au kaolewa.Huwa hazina utii wala upendo dhati. Ndoa ya aina hii
ikifikisha miaka 4 huwa hazivunjiki wahusika huishi kwa ajili ya mazoea na
watoto.
9. NDOA YA UPENDO.
Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya
kagera.Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu ila utu tu ambao uliwaunganisha
na kutengeneza upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.
10. NDOA KUCHUMA
Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji akapate kitu
au vitu Fulani(kama vile kazi,mali,umarufu,tenda) kutoka kwa mpenzi wake au
wakwe upande upande wa pili . Hii hudumu miaka kadhaa kutegemea na malengo ya
mhusika. Wengine husubiri mpaka mhusika afe,lakini hujikuta wanakufa wao
kwanza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni