Kuna dogo
mmoja rafiki yangu (sio kivile sana ila tunaangalia mpira pamoja) alikuwa anatembea na mke wa mtu kwa muda mrefu
tu, Ila mke ni mkubwa kiasi sana kwa mshikaji, mke ana kama miaka 37 hivi alafu
jamaa ana 30. Mume alikuwa bize sana na michakato ya kuboresha familia yake na
kiukweli alikuwa anaihudumia familia yake vizuri tu hasaa mpaka akafanikiwa
kumnunulia mkewe gari aina ya Harrier kwa ajili ya kutembelea nakuendea kwenye kitchen party,huku mwanaume akiendelea kusota
na madaladala kilasiku.
Kutokana na huduma nzuri na kamili ambazo mke
alikuwa anazipata hata muonekano wake kwa kweli ulikua unavutia hata huwezi
kumdhania kama yupo above 30 na tayari ana watoto 3, kwani alikua amejazia
vizuri tu wowowo limemwagika la haja tu ,nadhani matunzo mazuri na kutosimangwa
na mume kulimfanya azidi kunawili na kuwa mzuri ukichukulia kuwa pesa ilikwepo na hana
stress za daladala katikati ya jiji la
Dar es Salaam.Kipindi cha kampeni za uchaguzi mwezi uliopita alikua akivaa
gauni la chama kimoja cha siasa zile alama zilikua zikimkaa vyema kwenye
makalio yaani ilikua ni patashika barabarani kwa wapita njia na madereva wa
bodaboba na teksi!Macho hayana pazia!
Mahusiano yao sijui yalianzaje maana mimi
niliyagundua kwa bahati mbaya tu baada ya kuona picha ya yule mama kwenye simu
ya mshikaji akiwa amevaa bikini pekee, hapo nikapata mashaka na ndipo
nilipomuuliza mshikaji hapo vipi tena ? akawa hana namna ikabidi aniambie ukweli
wote, nikamshauri sana kukaa mbali na yule mwanamke kwani asije akahatarisha
maisha yake na nikamwabia mbaya zaidi nayeye ana mke kwanini anafanya hivyo?Alinijibu
kuwa namuonea wivu nikaona sio shida nikae zangu kimya na nikamwambia wazi kuwa
urafiki wetu uishie hapo maana mimi sitaki matatizo na najua namna mke
anavyouma,na nilimwambia hawezi maliza miezi sita bila ya kukamatwa akauliza kwanini?nikamjibu kuwa ni lazima
wataanza kujisahahu na kuhisi kuwa wapo
peponi na hakuna mtu atakayeweza kuona wanayoyafanya.
Imepita miezi kama mitatu hivi tangu hayo
yatokee juzi amefika ghetto macho mekundu anataka nimsaidie hata ushauri.
Nikamuuliza ushauri gani tena?
Akajibu
kwamba mwenye mke amegundua mchezo wa
mkewe akatega mtego akawanasa, alipowashika akawaambia wavue nguo zote wafanye
mapenzi huku akiwa anawarekodi video na kuwapiga picha nyingi nyingi pia na
kumfanyia mambo ya kinyama sana ila
hajaniambia ni mambo gani,(sina uhakika kama “alimuwowa” au la) Mume amemwambia
mshikaji amchukue yule mwanamke ampeleke aende kwao (kwa mwanamke) akaseme yote
yaliyotokea na akaseme kuwa anataka aoe yeye then ampeleke kwao (kwa mshikaji)
akamtambulishe kama mchumba wake(mke wa pili mtarajiwa) process za ndoa zianze
na yeye atatoa 50% ya gharama zote ili akafaidi vizuri moja kwa moja, ametoa
wiki 1 tu huo mchakato uwe umeanza otherwise atampeleka mahakaman maana
ushahidi wote upo au atasambaza picha na video.
Amenifuata
nimsaidie mimi sijui hata nianze wapi kumshauri, naogopa kumkashifu au
kumkumbusha ushauri wangu nahisi nitamuumiza.. Wadau tunafanyaje hapo?Daah mke
wa mtu nomaaa yaani sio kabisa maze.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni