Jumatatu, 1 Februari 2016

KWA WADOEZI WA WAKE ZA WATU PITIA HAPA!

Kuna dogo mmoja rafiki yangu (sio  kivile sana  ila tunaangalia mpira pamoja)  alikuwa anatembea na mke wa mtu kwa muda mrefu tu, Ila mke ni mkubwa kiasi sana kwa mshikaji, mke ana kama miaka 37 hivi alafu jamaa ana 30. Mume alikuwa bize sana na michakato ya kuboresha familia yake na kiukweli alikuwa anaihudumia familia yake vizuri tu hasaa mpaka akafanikiwa kumnunulia mkewe gari aina ya Harrier kwa ajili ya kutembelea nakuendea kwenye  kitchen party,huku mwanaume akiendelea kusota na madaladala kilasiku.
 Kutokana na huduma nzuri na kamili ambazo mke alikuwa anazipata hata muonekano wake kwa kweli ulikua unavutia hata huwezi kumdhania kama yupo above 30 na tayari ana watoto 3, kwani alikua amejazia vizuri tu wowowo limemwagika la haja tu ,nadhani matunzo mazuri na kutosimangwa na   mume kulimfanya azidi kunawili na kuwa  mzuri ukichukulia kuwa pesa ilikwepo na hana stress za daladala katikati ya  jiji la Dar es Salaam.Kipindi cha kampeni za uchaguzi mwezi uliopita alikua akivaa gauni la chama kimoja cha siasa zile alama zilikua zikimkaa vyema kwenye makalio yaani ilikua ni patashika barabarani kwa wapita njia na madereva wa bodaboba na teksi!Macho hayana pazia!
 Mahusiano yao sijui yalianzaje maana mimi niliyagundua kwa bahati mbaya tu baada ya kuona picha ya yule mama kwenye simu ya mshikaji akiwa amevaa bikini pekee, hapo nikapata mashaka na ndipo nilipomuuliza mshikaji hapo vipi tena ? akawa hana namna ikabidi aniambie ukweli wote, nikamshauri sana kukaa mbali na yule mwanamke kwani asije akahatarisha maisha yake na nikamwabia mbaya zaidi nayeye ana mke kwanini anafanya hivyo?Alinijibu kuwa namuonea wivu nikaona sio shida nikae zangu kimya na nikamwambia wazi kuwa urafiki wetu uishie hapo maana mimi sitaki matatizo na najua namna mke anavyouma,na nilimwambia hawezi maliza miezi sita bila ya kukamatwa   akauliza kwanini?nikamjibu kuwa ni lazima wataanza kujisahahu na kuhisi kuwa  wapo peponi na hakuna mtu atakayeweza kuona wanayoyafanya.
 Imepita miezi kama mitatu hivi tangu hayo yatokee juzi amefika ghetto macho mekundu  anataka nimsaidie hata ushauri.
Nikamuuliza ushauri gani tena?        
Akajibu kwamba  mwenye mke amegundua mchezo wa mkewe akatega mtego akawanasa, alipowashika akawaambia wavue nguo zote wafanye mapenzi huku akiwa anawarekodi video na kuwapiga picha nyingi nyingi pia na kumfanyia  mambo ya kinyama sana ila hajaniambia ni mambo gani,(sina uhakika kama “alimuwowa” au la) Mume amemwambia mshikaji amchukue yule mwanamke ampeleke aende kwao (kwa mwanamke) akaseme yote yaliyotokea na akaseme kuwa anataka aoe yeye then ampeleke kwao (kwa mshikaji) akamtambulishe kama mchumba wake(mke wa pili mtarajiwa) process za ndoa zianze na yeye atatoa 50% ya gharama zote ili akafaidi vizuri moja kwa moja, ametoa wiki 1 tu huo mchakato uwe umeanza otherwise atampeleka mahakaman maana ushahidi wote upo au atasambaza picha na video.

Amenifuata nimsaidie mimi sijui hata nianze wapi kumshauri, naogopa kumkashifu au kumkumbusha ushauri wangu nahisi nitamuumiza.. Wadau tunafanyaje hapo?Daah mke wa mtu nomaaa yaani sio kabisa  maze.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni