Nimefika kazini mapema leo kama kawaida yangu,najitahidi
kufanya kazi yaani hata mambo hayaendi nashika hiki mara naacha naenda uani
haja haipo narudi naangalia computer yaani
hakuna kinachosegea!mawazo tele moyoyni!Sasa nikiwa katika kutafakari
kuna jambo nimelikumbuka limenichanganya kidogo....
Huwa tuna kawaida ya kila weekends mimi na mke wangu
kufanyiana usafi ikiwemo kunyoana nywele za chini na makwapani. Huwa tunafanya
hivi weekends...
Sasa imepita kama mwezi hivi nilikuwa busy sana sikumnyoa.
Sasa jana usiku nimetoka kazini akaning'ang'ania nimnyoe na hakutaka kabisa
kusubiri weekend. Mzee mzima nikachukua kinyoleo nikaanza kazi huku namtania
tania na kumtekenyaa hapa na pale..
Sasa kinachonichanganya ni hiki. Wakati namyoa nikabakisha
vinywele flani nikamtania kuwa hivi tuviache nitamalizia weekend. Akanijibu..
"Mmmh malizia baby si nitaonekana kituko mie"
Nikashtuka kidogo alafu nikapotezea kwa kubadilisha stori nyingine, nikammalizia,
tukaoga tukalaa. .Sasa wakati natafakari mambo yangu hapa job ndo nikaimbuka
ile statement yake.
"Mmmh malizia baby si nitaonekana kituko mie"
Hivi sijui alimaanisha nini...ataonekana kituko na nani?
Mbaya zaidi nampigia hapatikani na nimeondoka simu yake ina
chaji full maana alitumia chaja yangu usiku mzima...
Sijui niombe ruhusa naumwa nirudi nyumbani?
Au shetani tu ananiletea mawazo mabaya?
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni