Habari zenu wapendwa,
Natumaini mpo salama
japo kwa upande wangu sipo salama sana nimechanganyikwa leo mbayaaaa!mpaka
ninavyoandika uzi huu nimeshindwa hata kwenda kazini na hapa moyo wangu unaenda
mbionaombeni msaada kwenu wa kiushauri
na wa kimawazo naweza hata mkanipoteza katika dunia hii kwa presha niliyokua
nayo hapa nilipo ,nimeshindwa hata kuwasha gari !akili zangu nahisi hazipo
timamu kwa sasa!
Ukweli ni kwamba nilikuwa naandika SMS kwa mchepuko wangu
uitwao Roswita au (mama Jane) na kwa bahati mbaya sana wakati natuma nikakosea
namba na kutuma katika namba ya mama mkwe wangu na meseji ikawa sent and
delivered.Kwenye simu yangu nimesevu jina lala Mama Jane sasa kwa kuwa jina
lipo karibu na jina la “mama mkwe” nikajisahau na kubonyeza sent alafu OK kwa
bahati mbaya!Nikajikuta tayari meseji ipo kwenye sent item na mara baada tu ya
kituma ghafla mama mkwe akanipigia zidi ya missed call ishirini hivi ila kwa kuogopa na aibu nimeona nisipokee na
nimezima simu kabisa.
Na kwa dalili ninazoziona ni lazima tu atakuwa
ameshamtaarifu na pengine hata kum-foward ile SMS mke wangu Magie maana nampigia
simu hapokei ila amenitumia meseji inasema “sasa ndo umefanya nini mume wangu!”
sasa sijui leo kama patakucha akiludi baadae maana ndo ameshakwenda kuwajibika tayari
kazini.
Meseji yenyewe niliyoituma ni hii " Mambo vipi Roswita
Bonita ! Hujambo? Umeamka salama? Vipi si tayari umeshamaliza period yako na
leo naweza kuja ukanipa mambo love?unipe na ile tamu tamu honie!Zingine
nizibakize kwa dada yako “baby wife” wangu maalum kwa siku ya Valentina Jumapili hii kwani ni haki yake ya kindoa.
Utaninunulia Wine gani leo ili nikuchangamshe vizuri kama unavyopenda?Honie
usisahau na yale mafuta basi!Baby uvae ile bikini ya purple na mechisha na ile
bra yake! Halafu ulisema unataka hela sijui ya kununua nguo ila kwakuwa ili li
mke langu nalo eti linataka hela sasa ngoja kwanza nilidanganye kuwa sina na lisubiri
hadi nipate ila wewe mke mdogo nakutumia
sasa hivi sawa? Si ulitaka Tsh laki 1? Sasa nakutumia Tsh Laki 2 na nusu hizo
zingine utajua utanunua nini au utaitumiaje sawa baby?
Nijibu na tambua sitokuacha
kamwe mwaaaaaah Loswita ".
Hiyo ndo meseji niliyotuma najua kimeshanuka sijui
nikimbilie wapi?Nilipiga simu kwa jamaa yangu yupo Telecom company ikiwezekana
aisimamishe iyo meseji hewani nimpe hata laki tano imeshindikana kabisa!mnijibu
haraka basi ili niweze jipanga kuzipangua hoja kama hali ikiwa mbaya kweli.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni