Jumatatu, 1 Februari 2016

WANAWAKE MNAOPENDA KWENDA KWA WAGANGA WA KIENYEJI SOMENI HAPA!

Kuna jamaa mmoja namfahamu anapenda sana ngono na pia ana uwezo mzuri kipesa, sasa kuna wadada wengi alikuwa akiwatamani sana ila kuwapata ikawa ni ngumu kwasababu domo zege  alafu mvuto hafifu,alichofanya ni kwenda hadi kwa mganga mmoja maarufu sana ambaye wanawake wengi hupenda kwenda kwake, akampatia yule mganga mshiko wa maana  na kumwomba kuwa kila mwanamke mrembo anayefika kwake aidha kutafuta dawa ya kupata mchumba awe anaambiwa na mganga kuwa, ukitoka hapa mwanaume utakayekutana nae njia panda wa kwanza kukusemesha ,usimkatae maana huyo ndo anapata na mzimu wako wa mafanikio na uhakikishe umetembea naye tena ikibidi siku hiyo hiyo utafungua njia ya bahati katika mapenzi.
Baada ya kupanga mikakati yote na yule mganga, jamaa akawa anabana sehemu ya njia panda na  kusubiri mwanamke anayetoka kwa mganga na tayari wanakuwa wamefanya mawasiliano na mganga juu ya ujio wa uyo mrembo!, jamaa tayari kamaliza mabinti kibao!
Anakuwa amevalia mavazi tofauti tofauti  ili asitambulike na ana laini kibao za simu, anahakikisha kuwa kawalala siku hiyo hiyo.


Wadada mgeukieni Mungu kwa shetani hakuna kitu zaidi ya mauti.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni