Kuna jamaa mmoja namfahamu anapenda sana ngono na pia ana
uwezo mzuri kipesa, sasa kuna wadada wengi alikuwa akiwatamani sana ila
kuwapata ikawa ni ngumu kwasababu domo zege alafu mvuto hafifu,alichofanya ni kwenda hadi kwa mganga mmoja maarufu
sana ambaye wanawake wengi hupenda kwenda kwake, akampatia yule mganga mshiko
wa maana na kumwomba kuwa kila mwanamke
mrembo anayefika kwake aidha kutafuta dawa ya kupata mchumba awe anaambiwa na
mganga kuwa, ukitoka hapa mwanaume utakayekutana nae njia panda wa kwanza
kukusemesha ,usimkatae maana huyo ndo anapata na mzimu wako wa mafanikio na
uhakikishe umetembea naye tena ikibidi siku hiyo hiyo utafungua njia ya bahati
katika mapenzi.
Baada ya kupanga mikakati yote na yule mganga, jamaa akawa
anabana sehemu ya njia panda na kusubiri
mwanamke anayetoka kwa mganga na tayari wanakuwa wamefanya mawasiliano na
mganga juu ya ujio wa uyo mrembo!, jamaa tayari kamaliza mabinti kibao!
Anakuwa amevalia mavazi tofauti tofauti ili asitambulike na ana laini kibao za simu,
anahakikisha kuwa kawalala siku hiyo hiyo.
Wadada mgeukieni Mungu kwa shetani hakuna kitu zaidi ya
mauti.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni