Wadau mambo
vipi?
Kuna jambo
limeikoroga akili yangu sana juzi naomba niwashirikishe kidogo. Jumamosi
iliyopita mimi na wife tulienda kula bata maeneo ya Villa Park hapa Mwanza nyakati za jioni baada ya kutoka
kufanya shopping hapo Rock City Mall maeneo ya Ghana. Wakati tumefika maEneo ya Nyegezi
tukielekea mjini wife alinambia nisimame kidogo kuna rafiki yake yupo saloon ambaye
nilikua namfahamu tangu wakiwa chuo Saut
Nyegezi , nae alikua anaelekea hukohuko Rock cCity Mall tumchukue,
akampigia girlfriend simu aje barabarani . Hivyo tukawa watatu kwenyegari mpaka
mizunguko ya huko mall; mimi, wife na
girlfriend ambae alikua family friend kwetu ingawa mimi sina mazoea nae
kiiivile.
Kwa kuwa
ilikua mida ya saa kumi na moja jua lilipoanza kuzama tukaamua kukaa Villa Park
kwa ajili ya kusubiri kusakata rhumba na kwa kuwa wwife huyu alikua ni shaga
yake hasa sikua na option zaidi ya kuwaacha wahe huru uku mimi nikiendelea
kugonga Konyagi yangu kubwa na better lemon
na wao walikua wanakunywa Saint Anna moja wawili, tukakaa karibia na
kaunta ya chini nje. Kwenye saa mbili
kasoro usiku akajitokeza jamaa mmoja kwa sura simjuhi kabisa ,baada ya kutuona
akaja kutusalimia, ambapo wife aliinuka kwa shangwe kubwa na kumlaki kwa hugs
na zile kiss za mashavuni wanazopiganaga wale wanaojifanya wazungu,jamaa
likamkumbatia wife kwa nguvu.Nilipata kawivu kidogo lakini nikajikaza kiume!
Wife
akanitambulisha kuwa "he is a longtime friend,huku nikiendelea kumtazama
kwa mashaka kwani nilihisi zile mbwe mbwe zote za kukumbatiana pale kuwa sio ‘genuine’
lazima kuna kitu au kulikua na kitu fulani zamani,haiwezekani,hamna hapana!kuna
kitu tu!". Jamaa akaita weita na akazungusha mbili za vinywaji, alafu
akaniomba aende akamtambulishe wife kwenye meza yao kwa rafiki zake
,sikupendelea hiyo hali lakini kwa kuwa nilimuona wife ana muhemko fulani wa
bashasha ya kukutana naa “friend wa zamani” nikakubalitu kwa shingo upande ingawa moyoni nilikua nimefura kwa hasira,
sema sikutaka kuonesha, bahati mbaya zaidi meza ya hiyo aliyokua ametokea huyo
jamaa ilijaa wanaume pekee.
Tukabaki
wawili wakati wife anaongea na meza ile, yule girlfriend akasema "shemeji
naomba namba yako hapa mjini huwezi kujua ya kesho na keshokutwa", nami
nikajibu ni kweli kabisa, tukabadilishana namba.Monday yule binti akanipigia
simu nikiwa kazini akaniambia shemeji kuna jambo nataka kukuambia ila
usinitaje, nikajibu poa, akasema, "Yule jamaa wa jana ni ex wa mkeo.
Walikua wapenzi kwa miaka yote mitatu chuoni wakiishi chumba kimoja nje ya chuo
kama mke na Mume".
Na kwamba
kwa kipindi chote cha hiyo 3 yrs alitoa kama mimba 2 hivi za huyo mshikaji, pia
uhusiano wao ulienda hadi mtaani after university life. Walikuja kuachana kila
mtu alipopata kazi yule ndugu akapelekwa Songea. Since then hawajawahi kuonana
hadi hiyo jumapili pale Lock City Mall,Mwanza na kwamba ile njemba limerudishwa
hapa Mwanza na halijaoa bado ila lina mapene sana.
Binti huyu
alinibembeleza sana kuwa nisimtaje kabisa kama yeye ndie source ya hiyo habari.
Huyu binti ni rafiki wa wife tangu chuo ila bahati mbaya ndoa yake ilipata
shida kidogo na kushindikana kutokana na uzinzi wa mwanaume.Niliporudi home
jioni ya monday nikaamua kulianzisha, ambapo wife alidai hakuona busara
kunitambulisha kwamba yule bwana alikua ex wake.
Nikamuuliza
ilikuaje ukafurahi na kushangilia kiasi kile na kushindwa kuficha kabisa hisia
zako? Akabaki anajiuma uma tu na kushindwa kujibu.
Kiukweli
sijaridhika na majibu yale na bado nafanya uchunguzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni