Jumatano, 6 Januari 2016

MKE WANGU ALITAKA KUNIBAMBIKIA MTOTO!

Wadau,Mimi na mke wangu tumekua na ugomvi wa muda mrefu kuhusu nani amfuate mwenzake,maana tunafanya kazi katika mikoa tofauti mimi nikiwa Kigoma na yeye akiwaDar es Salaam.Suala la uhamisho lilishindikana kutokana na mahali anapofanyika kazi wife kutokuwa na Ofisi katika Kanda ya Ziwa.Solution ilionekana ni wife kupiga kazi chini ili tuweze kuishi pamoja.Na kutokana na changamoto za maisha ilikua ni gharama sana kupanda ndege isitoshe umbali wa Kigoma to Dar kwa basi ni kama siku moja na nusu na ukikata tiketi ya ndege ya bei nafuu lazima uwe umefanya booking hata wiki nne kabla ya safari na huku huwezi jua kama iyo ruhusa utapata ofisini au la.
Ikafika mahali tunamaliza hata miezi minne mpaka saba bila ya kuonana na mama mkwe wangu alikua anambembeleza sana wife akubali kuacha kazi ili anifuate Kigoma tuishi,na kwamba ndoa za mbali matatizo huwa hayaishi lakini wife aliendelea kushikilia uzi kwa kusema ajila yake ndio mume wake wa kwanza!
Baada ya kuendelea kusimamia misimamo yake ilibidi nitafute mtu wa karibu anayeweza kunipa taarifa za kiintelijensia kuhusu wife  na kumbuka muda wote huo alikua anaishi nyumbani kwa wazazi wake,nilimweka kwa ukaribu sna binamu yake wa kike awe ananipa taarifa za kilasiku sana sana wikiendi anarudi saa ngapi nyumbani.
Mojawapo ya taarifa nilizokuwa napata ni mwenendo wake wa kupenda kujipamba sana wikiendi na kutoka outing na kurudishwa mida mibaya na mtu asiyejulikana akisingizia partyie za ofisini na mikutano ya mara kwa mara.Kilichonishtua zaidi ni mwenendo wake wa kuvaa nguo fupi ghafla tena wikiend ambapo haikua sehemu ya tabia yake.Siku za kazi alikua anarudi saa nne usiku akisingizia foreni .Hata ivyo sikuwa na papara  kwa taarifa hizo kwani kugoma kwake kuhamia Kigoma nilichukulia kwa uzito mkubwa nikidhani kutakua na  sababu za  msingi labda za kifamilia ukweni .Nikajisemea moyoni siku za mwizi therathini na tisa ya arobaini udakwa tu.
Katikati mwa mwezi wa kuminambili mwaka jana wife alinipigia simu kuwa amekubali kuacha kazi kunifuata Kigoma,tena anataka kuja ndani ya wiki tu,nilishangaa imekuaje muda wote alikataa mbona ghafla kabadilisha mawzo!Nikawaza sana nikasema haiwezekani kuna kitu tu!Nikainua waya na kumpigia shushu wangu cousin wake,lilikua jipu hatari!Aliniambia mkeo ana mimba changa,anataka aje akupe mara moja mbili aseme ni ya kwako!kitu ambacho ni kwelie maana wife alikua na haraka mno ya kuja tena kwa kukata tiketi ya ndege yeye mwenyewe!
Lakini wakati yote hayo yanatokea wiki hiyohiyo likizo yangu ikapita kwa bosi nikaruhusiwa,niliomba December iligoma wiki ya kwanza ya January ikakubaliwa nikapewa wiki mbili wakati wife anajiandaa kuja nikachukua fast jet jioni nipo Sinza kwao.
Nilipofika tu nikaanzisha kesi mbele ya wazazi wake kuwa twende wote mguu kwa mguu tu kacheki mimba hospitali ambapo ni mtaa wa nyuma tu kutoka kwao,akagoma na kuanza kulia,mama mkwe alikua ameina tu chini.
Wote walikua wanajua kuwa mimi na wife tuna mwaka bila ya kuonana hivyo hiyo si mimba yangu na mama mkwe alilijua hilo na akavunja ukimya hapohapo kwa hasira na kumwambia mwanae kuwa "si nilikwambia uache kazi umfuate mumeo ukaniona mimi wa zamani,siwezi kushiriki dhambi yako kumbambikia huyu bwana mtoto,maadamu keshastuka mwache ajue tu,baba ni kweli ana mimba huyu kama ulivyosema".
Ndoa yetu ikawa imeishia hapo,taarifa zilizopo ni kwamba aliitoa mimba hiyo na bado yupo kwao,ingawa haendi kazini sijajua kilitokea nini,hadi sasa ameshatuma waze wengi kuja kwangu kuzungumza turudiane,wakiwemo ndugu zangu,ila bahati mbaya nimeshamfuta  mazima moyoni,ataisomaga namba.  

Maoni 1 :

  1. Huu ni lazima ushuhudia usomaji na kila mtu, nipo hapa kuruhusu ulimwengu wote kujua kuhusu mtu aliyeokoa uhusiano wangu na mtu huyu mkuu anaitwa Dr IZOYA. Hakika alifanya kazi nzuri kwangu kwa kumrudisha mpenzi wangu wa zamani ambaye aliniacha na kuahidi kamwe kurudi kwangu tena. Kwa hili, nimekuja kutambua kuwa kutoa maelezo ya Dk IZOYA kwa ulimwengu utafanya mengi mazuri kwa wale walio na nyumba zilizovunja au uhusiano kwa ajili yake ili kukusaidia kurekebisha uhusiano huo uliovunjika au ndoa yako. Unaweza kumfikia kupitia anwani yake ya barua pepe: drizayaomosolution@gmail.com au kumwita moja kwa moja kwenye [+12098373537]. Kuwasiliana naye na kuona jinsi tatizo lako litatatuliwa ndani ya 24hours. Pia mtaalamu katika mambo yafuatayo ...
    (1) Unataka kurudi nyuma yako.
    (2) Unataka kukuzwa katika ofisi yako.
    (3) Unataka wanaume / wanawake kukufuate.
    (4) Unataka mtoto.
    (5) Wewe ni mjasiriamali na unataka kushinda mikataba
    (6) Unataka mume wako awe wako milele
    (7) Unahitaji msaada wa kiroho.
    (8) Umeshambuliwa na unataka kupona fedha zilizopotea.
    (9) Weka talaka
    (10) Kualika kwa mila ya fedha
    (11) Chagua uchaguzi

    JibuFuta